Muongozo wa baraza hilo umesema Waislamu wanaruhusiwa kutumia chanjo ya COVID-19 kwani ni hitajio muhimu la kulinda maisha wakati huu w janga la COVID-19.
Taarifa hiyo imesema kwa ujumla mchakato wa utegenezaji wa chanjo ulizingatia mafundisho ya Kiislamu na kuongeza kwamba Uislamu unalipa umuhimu mkubwa suala la maisha hivyo ni muhimu kutumia chanjo hiyo.
Waziri wa Masuala ya Kidini Singapore Masagos Zulkifli amekaribisha muongozo wa Muis na amewahimiza Waislamu wachanjwe punde chanjo hiyo itakapopatikana Singapore.