IQNA

Kikao cha Dharura cha OIC kujadili hujuma za Israel al Aqsa

20:50 - September 20, 2015
Habari ID: 3365554
Jumuiya ya Ushirikiano wa nchi za Kiislamu OIC imeitisha kikao cha dharura cha mawaziri wa mambo ya nje wa nchi wanachama kujadili hujuma za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Msikiti wa al Aqsa katika mji wa Quds.

Katibu mkuu wa OIC Iyad Madani amesema ofisi yake inawasiliana na nchi wanachama kwa lengo la kuitisha kikao pembizoni mwa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York baadaye mwezi huu.
Amesisitiza kuwa mutano huo ni muhimu na wa dharura kwa kuzingatia hujuma zisizo na kikomo dhidi ya Msikti wa Al Aqsa na njama za kuugawa msikiti huo.
Wachambuzi wa mambo wanaamini kwamba, Baytul Muqaddas na Msikiti wa al-Aqswa sasa vinakabiliwa na duru mpya ya vitisho na njama za utawala wa Kizayuni wa Israel ambapo moja ya njama hizo ni mpango mchafu wa utawala huo ghasibu wa kutaka kuugawa msikiti huo katika sehemu mbili za Wapalestina na Wazayuni na kugawa pia nyakati za kuingia na kutoka katika msikiti huo. Katika mazingira kama haya ya njama mtawalia za Wazayuni maghasibu dhidi ya msikiti wa al-Aqswa, bila shaka kuna udharura kwa Wapalestina, Waislamu na jamii ya kimataifa kuonyesha radimali zao za kukabiliana na njama hizo za Wazayuni za kila siku iendayo kwa Mungu.
Masjidul Aqsa ni kibla cha kwanza cha Waislamu na eneo la tatu kwa utukufu baada ya Masjidul Haram mjini Makka na Masjidun Nabawi mjini Madina huko Saudi Arabia.

3365174

captcha